Monday, January 28, 2008

KWA NINI ULIENDA SHULE? KWA NINI UNASOMA?


Huu ni ushauri wangu, siuzi, usiogope kuuchukua kwa kudhani utagharamia kitu!



Niseme mapema, mimi si mwandishi mahiri wa makala, kwa hiyo usitarajie mtiririko mzuri kama ule wa waandishi mahiri nchini, lakini zingatia zaidi ujumbe.

Naandika makala hii kwa uchungu utokao kutoka kilindi cha moyo wangu. Naandika pia kwa majonzi makubwa nikiwa njia panda nisijue hatima ya jambo Fulani nitakalokueleza muda si mrefu ujao katika makala hii.

Nina swali ndugu zangu, swali langu ni hili; kwa nini tunaenda shule? Sijauliza kwa nini tulisoma? Hapana nimeuliza “kwa nini tunasoma” Swali hili haliwahusu wale ambao tayari wako maofisini, wanafanya biashara, mawaziri na wabunge. Swali langu ni kwa wale tu ambao bado wako mashuleni na hasa vyuoni, hususani vyuo vya elimu ya juu au vyuo vikuu. Hawa ndio walengwa wangu hapa.

Nimewahi kukaa na wanafunzi, ninapokutana nao kwenye daladala, shuleni, mitaani na hata wale ambao huja kunitembelea na kuwauliza swali hili. Wengi wao wamenijibu jibu ambalo hata wewe ambaye unasoma makala hii pengine ungelitabiri na kupatia au kunijibu. Wameniambia kwamba wanasoma ili waje kuwa na maisha mazuri hapo baadae, wapate kazi nzuri, basi, wakishapata kazi nzuri yatosha.

Na si ajabu watakwambia kwamba wanasoma ili wapate kazi Benki kuu, T.R.A, Ikulu, au kwenye wizara mbalimbali ambako wanafunzi hutiana moyo kwamba kuna kazi na maslahi mazuri. Wanasahau kwamba tuna wasomi wengi mitaani waliochoka kimaisha, wanaosota kwa kukosa ajira, lakini hawasumbui akili zao kujiuliza ni nani anasababisha ajira zisiwepo. Je katika kusababisha uhaba huo wa ajira, hakuna wanaoitwa wasomi? Tunajua kuwa serikali haina ajira zote, lakini ina uwezo wa kuandaa mazingira ya uwepo wa ajira kwa wananchi wake, nini kimetokea? Na kasababisha? Je, wasomi hawahusiki humo?

Wachache huwaza kusoma ili wawe walimu wa sekondari na msingi, hilo huliweka mwisho tena ikitokea wakafeli. Kaa na mtanzania mwenzako, muulize kwa nini anasoma? Sikiliza jibu lake, litafakari jibu hilo kisha pambanua na kuona usahihi wake.

Wengine wapo tu, wanasoma ili waje kuwa wazungumzaji wazuri wa Kiingereza (lugha ya kikoloni) kwao ni ufahari kuzungumza kiingereza kuliko Kiswahili, usipojua kiingereza unaonekana mshamba, unaonekana huna akili timamu, waulize wanafunzi wa vyuo vikuu watakwambia hili. Ni watumwa wa kingeereza, wanasahau kwamba kingereza ni lugha kama kinyakyusa, kingoni, kisukuma, kichaga na zinginezo. Wanasahau au hawajui kwamba kutokujua kingereza ni haki ya mtanzania mzawa wa hapa, si dhambi maana hawakuzaliwa nayo!

Wengine wanasoma ili nyumba zao baadae zipambwe na vyeti vya shahada na stashahada ukutani, hilo tu basi! Wanasoma ili na wao watembee vifua mbele wakiwa wanaitwa wasomi mitaani, waitwe mainjinia wakati mitaa yao inatiririka maji machafu kama ile ya Sinza kwa kukosa mitaro ambayo tulitegemea wasomi hao watumie taaaluma yao kutatua tatizo hilo. Wanataka waitwe wasomi mitaani wakati baba zao, mama zao, kaka na dada zao vijijini wanadhulumiwa mazao yao kwa kulazimishwa kuuza mazao kwa bei isiyowakwamua kiuchumi.

Wanataka waitwe wasomi wana sheria wakati wameshindwa kabisa kutetea mahabusu ambao pengine kesi zao zinacheleweshwa bila sababu za msingi, wameshindwa kutatua tatizo hili sugu. Wanataka waitwe wana habari wasomi huku wakiwa wameigeuzia kisogo jamii yao kwa kukubali kupokea pesa ya bia (rushwa) kuliko kuandika habari za kufichua ufisadi nchini, wanakubali kuisaliti jamii ya wasio na sauti kwa kuhongwa ili kuwaandika vizuri wanasiasa wanaowanyonya mamilioni ya watanzania masikini kwa uroho, ubadhirifu na dhuluma! NK

Hapa najiuliza, nini tafsiri ya msomi? Msomi ni nani? Je, tumwite mtu msomi kwa sababu kahitimu miaka mitatu ya masomo yake Chuo Kikuu cha Tumaini, Mlimani, Mzumbe au Mtakatifu Augustine wakati hana mchango wowote kwa jamii yake zaidi ya kuisaliti? Kwa hali ilivyo sasa, kwa wasomi kushindwa kutumia taaluma zao kututatulia matatizo katika nchi hii, jamii inawalaani, hivyo kuitwa msomi ni kama laana au kujilaani. Kwamba ni laana kuitwa msomi katika nchi hii.

Sasa kwako wewe uliyeko shuleni, kwa nini unasoma? Kwa nini umeamua kusomea fani unayosomea? Je, ni kwa vile wazazi au rafiki zako wamekushinikiza? Je, ni kwa sababu unataka kujipatia viza kwenda kuishi London, New York, Amsterdam? Kisha iweje? Je, unasoma ili upate kazi nzuri? Fikiria mtu kama Daud Balali, aliyekuwa gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (B.K.T) si alikuwa msomi? Kazi yake si ilikuwa nzuri? Amelifanyia nini Taifa? Tafakari!

Sikiliza, nataka nikushawishi, nataka nikugeuze fikra zako leo, kama ulikuwa unasoma kwa ajili ya mambo hayo hapo juu badilika. Tunataka mapinduzi. Hii ni kwa ajili yako wewe uliyeko shule, hata wewe utakaye hitimu hivi karibuni, hujachelewa, bado una muda wa kubadilika.

Nataka nikwambie kwamba kuanzia sasa, kama ulikuwa hujui basi ANZA KUSOMA KWA AJILI YA TANZANIA. SOMA KWA AJILI YA TAIFA LAKO.

Kama vijana wa Tanzania wanasoma kwa ajili tu ya kupata pesa za kula wao na familia zao basi niko njia panda. Maana hii ni ubinafsi na hatima ya Taifa letu iko mashakani. Unaweza ukadhani nakurudisha kwenye zama za ujamaa, lakini ukweli ndio huo!

Sikiliza kijana, Taifa linakusubiri, watanzania wanakusubiri! Si kwamba usome ili uje uwamwagie mapesa, lahasha, wanataka wasomi wa kizazi kipya, wasomi waadilifu, wenye moyo wa uzalendo, si wale wanaolitumikia Taifa huku wakiwa na urai wa nchi mbili, ili kwamba baada ya kuwaibia watanzania waukane uraia wa Tanzania. Taifa linakungoja, soma ili uje ulikwamue kutoka katika matope lilipokwamishwa na wasomi wabinafsi, waliosoma ili wapate kazi/ajira nzuri.

Fikiria kuhusu aliyekuwa waziri wa Fedha wakati wa awamu ya tatu, Basil
Mramba, aliyetangaza bila huruma, bila aibu kwamba ni bora watanzania wale nyasi lakini ndege ya rais inunuliwe, je, hayakuwa matusi kwa watanzania? Je, Mramba si msomi? Usomi huu una tija kwa watanzania? ‘sitaki kuamini kwamba aliyasema haya akiwa amedhamiria kuwatukana watanzania’

Fikiria kuhusu wabunge wasomi walioko kwenye bunge la jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao huelewa fika kwamba wanaposimama na kutetea itikadi za vyama vyao kuliko maslahi ya Taifa katika kufikia maamuzi mazito ya mustakabali wa Taifa hili ni kuturudisha nyuma kimaendeleo. Watanzania (hata kama hawasemi) mioyo yao ina shauku ya kuwa na wasomi watakaoweka mbele utaifa kuliko u-CCM, u-CHADEMA, u-CUF, u-TLP nakadhalika! Hii ndio shauku ya watanzania! Ni wewe uliyeko shule ukikubali kubadilika na kuweka utaifa mbele.

Taifa letu ni sawa na kwamba limeuzwa, nani atalikomboa? Kila kitu wamepewa matajiri wa nje, utamaduni wetu umeuzwa, uadilifu, utaifa, mashirika, viwanda, madini, pengine bado sisi tu kuuzwa. Ni wewe uliyeko shule usome ili kuwamilikisha uhuru halisi watanzania. Inawezekana kama utaamua. Ukiwa mbinafsi mwendo ni uleule, sote kulitumbukiza taifa hili shimoni, na maendeleo tutayasikia kutoka uropa na marekani.

Soma kijana, soma mtanzania, mama, baba, dada, kaka zako wanakusubiri uje utumie taaluma yako ya sheria kuja kusababisha sheria za kibabe/onevu kufutwa, uje utumie taaluma hiyo hiyo kufuta sheria mbovu za madini zinazowawezesha mabepari kufaidi urithi wetu wa madini tuliokirimiwa na Mwenyezi Mungu. Soma ili uje utumie taaluma yako ya udaktari kuwahudumia watanzania kwa moyo safi, wa huruma na uadilifu, maslahi yatakuja tu! Soma ili uje utumie taaluma yako kulinusuru Taifa hili. Yaliwezekana kwa wazungu yatawezekana kwetu pia, tuamue tu.

Tusome kwa ajili ya Taifa, weka uzalendo mbele. Hata kama unapanga kuwa mwasiasa baada ya kuhitimu, waza kuwa mwanasiasa kwa ajili ya Tanzania na sio CCM au chama kingine chochote, vyama hivyo viwe njia tu lakini si hatima, ndio maana naunga mkono harakati za kuruhusu wagombea binafsi wa ngazi mbalimbali za uongozi katika nchi hii.

Ukiniuliza mbona viongozi wetu wa leo ni wasomi mahiri lakini nchi bado iko nyuma, nitakuambia kwa urahisi tu kwamba walisoma ili wapate kazi nzuri, si kwa ajili ya taifa lao, kama sivyo niambie nini kimetokea? Nini kimewakwamisha? Hapana shaka kwamba tuna viongozi wabinafsi japo ni wasomi. Fikiria tena kuhusu watuhumiwa wa ufisadi BOT, walio tajwa na ambao bado hawajatajwa bado, wengi ni wasomi wazuri walioaminiwa kututumikia. Lakini walichotufanyia wewe na mimi tumekiona!

Nina mengi ya kusema, nikipata nafasi tena nitayasema.
Kwa mara nyingine tena, nataka nikwambie kwamba kuanzia sasa, kama ulikuwa hujui basi
ANZA KUSOMA KWA AJILI YA TANZANIA, SOMA KWA AJILI YA TAIFA LAKO! Kila la heri!

0713 550 778
Barua pepe: ilovejesustz@yahoo.com

Monday, January 21, 2008

LETTER FROM NAIROBI

Praise the Lord my brother. Things are not all that bad here in Kenya. We believe in God that all will be under control, and that our nation is not bound to fall.
We have learnt that the international community is getting very sad reports on what is happening here in Kenya; this is causing even our people overseas to get worried of our safety here in Kenya.
Please my brother you can help us pray to our Mighty God that He bring sanity in the minds of the people of Kenya especially the politicians who are inciting people into tribal conflicts.
There are those Kenyans who were once leaving happily with their neighbors, but now the same good neighbors’ turn against them just because they are not of their tribes, these people now are help in camps, with no food, shelter and proper sanitation.
Can you feel what this woman feels? It's like she says, "why you politicians doing this to us?"


This is the letter I have received this morning from a Kenyan friend of mine ( Paul) What he is trying to tell us in the first part of his letter is that, Kenya is not swimming in such a deep conflict as Media have been reporting. That Media manipulate the real bad event into worse.
According to BBC, over 600 peopled were killed particularly in Coastal, West, Nyanza, Nairobi, Rift Valley regions.

But again Paul admits that the situation is not so good, and that the same Kenyans who were living neighborly and brotherly are turning against each other. They are now hating and smashing one another.
Paul’s blames are strongly directed to the Politicians, who are stirring people to fight each other. Paul confess that there Kenya who are no living in camps, basically there are now treated as refugees in their own land, hence it simply verifies that Kenya is not okay!

From the letter, I want to remind Mr. Paul that no matter what is happening in Kenya recently, the World know that Kibaki furious friends have entered Kenya where it is now. What ever the state Kenya is, even what we call the false reports of the Media to the International community, Kibaki is the source.
Apart from praying for peace in Kenya, we have also a task to pray for sanity in people like Kibaki, who was supposed from the beginning to settle the matter by sitting in the same round table with ODM who seem to be given chance by Kenyans. God is faithful; he can do what we ask Him in his will.

The problem is clear, that Kibaki worship to be a life president of Kenya, yet people (some) want changes in their country. Kibaki may claim to love Kenyans and that is why he is forcing to lead them to the land of honey and milk, if letting people dying as flies, as the World witness now, then Kibaki’s love to Kenya is a the unexplained love from vacuum.
He would demonstrate his love by stepping down from his post as ‘president’ after the first death report due to disputed election results given out by Kivuitu’s KEC.

We are still insisting that we the none-Kenyans can not decide for Kenyans, but we can advise what to be done, because what is happening in Kenya can even reach in our lands by one way or another.
So to cement on these comments to the Paul’s letter, I can easily ask for Mr. Kibaki and his companionship to have pity on Kenyans.

Finally, below is the song done by the late Lucky Philip Dube, the song is titled by ‘POLITICAL GAME’

Thanks, GOD BLESSES AFRICA!


How do you feel when you lie?


Straight faced while people cry


How do you feel when you promise something


That you know you'll never do


Giving false hope to the people


Giving false hope to the underpriviledged


Do you really sleep at night?


When you know you're living a lie


To you it is just a job


To the people it hurts to the bone


ChorusOoh political games that they play x 4


What do you say to the orphans?


Of the women and men you sent to war


What do you say to the widows?


Of the men you sent to war


Telling them it is good for the country


When you know it's good for your ego


What a shame.Do you really sleep at night?


When you know you're living a lie


You talking tough, you talking sincerely


Giving false hope to the infected


Giving false hope to the affected.


To you it is just a jobTo the people it hurts to the bone.




Friday, January 4, 2008

MWAI KIBAKI WAHURUMIE WAKENYA!

Hebu soma sura za wananchi hawa, mwangalie huyu aliyevaa shati ya bluu na anayemfuatia kulia, mwenye kapero. Unadhani wanaimaba ujumbe gani? Au wanasema nini?
Utafanya makosa kudhani kwamba haya mawe yalijipanga hapa, ni wananchi kuashiria kwamba 'enough is enough'

Unaona huo ujumbe kwenye kifua cha kijana huyu? Anasema "tumechagua mabadiliko na sio mauti" Huu ni ujumbe wa umma, Umma unazungmza unasema unataka mabadiliko. Wanasiasa ni vema wakawa na busara, wananchi wakisema NO, iwe No!








Kwa muda mrefu nimekuwa kimya, wengi walitarajia pia kuona nini maoni ya wachambuzi mbalimbali wa masuala ya kisias kuhusu uchaguzi mkuu nchini Kenya.







Ningeweza kutoa maoni yangu mapema sana, lakini kwa kweli kilichonichelewesha ni bumbuwazi, masikitiko, huzuni na kila kinachofanana na hayo. Kinachousikitisha moyo wangu hasa si mauaji yanayoendelea nchini Kenya, bali ni kile ambacho akili yangu inaamini kuwa ni jeuri, kiburi na kutokujali kwa ndugu Mwai Kibaki.







Kibaki anajaribu kutka kuwa mmoja wa Madikteta waliowahi kuwapo Ulimwenguni. Kinachonifanya niamini haya si kwa sababu Kibaki ameshinda kiti cha urais, ushindi ambao ni tata, bali ni kitendo chake cha kukaa kimya na kuonekana kama mtu asijua kinachoendelea Kenya! Haonekani kuguswa na tatizo lililopo, na kama ni hivyo basi ni kwa maslahi ya kiti chake, kwamba kama wakenya wameweza kuzuia magari ya polisi njiani, basi kwa njia yoyote wanaweza kufanya lolote kubatilisha ushindi wake wa kizungumkuti.







Nimegusia suala la udikteta, kwa vile naamini kwamba mbali na sifa ya kutawala kibabe inayopamba udikteta, hali ya kutokujali usalama wa raia na kukosa huruma kwa wananchi ni sifa pia za udikteta.







Uchaguzi Kenya uliofanyika tarehe 27 Desemba 2007 ulianza kwa kasoro nyingi ikiwamo malalamiko kuhusu utaratibu mbovu wa orodha ya wapiga kura, kwa maelezo kwamba ilikuwa vigumu kupata majina ya waliojiandikisha. Mmoja wa wahanga wa hali hiyo ni mgombea urais wa chama cha ODM Bwana Raila Odinga.







Hata hivyo kwa wale waliokuwa wakifuatilia uchaguzi huo kwa karibu wanakumbuka kwamba kadri zoezi la uhesabuji kura lilivyoendelea ndivyo dalili za kushinda kwa Odinga zilivyoongezeka. lakini ghfla tukasikia kuwa mshindi si Odinga bali ni Kibaki ambaye kwa mujibu wa Tume ya Uchaguzi nchini Kenya ECK, anaiongoza Kenya kwa kipindi kingine cha miaka mitano.







Tukashituka lakini tukatulia tena kwamba tume imetangaza, lakini kwa kweli waliokuwapo huko hasa wakenya wenyewe, aksema NO, wakakataa kivitendo, ghasia zikazuka, naam hata sasa watu wanakufa, polisi kwa raia nao wameuwawa.







Kinachonisikitisha mpaka sasa ni kwamba Kibaki ni Mroho wa madaraka, nasikia amekataa usuluhishi, jambo ambalo tuliliombea sana, Kibaki analazimisha kutawala wakenya waliomkataa, ndivyo inavyoonesha. Na kinachoniumiza zaidi ni kwamba sijui anajisikiaje kuona mauaji yanvyoendela huko. Kwa nini asiachie tu ngazi na ikibidi kuitisha uchaguzi mwingine kama kweli ana uchungu na Wakenya. Kwa nini askubali kufanya mazungmzo na Odinga kama kweli si Dikteta?







Anafurahia mauaji ya watu ambao wamesema inatosha kwa yeye kutawala? Kama ana uhakika na ushindi wake kinachochelewesha kuunda tume ya uchunguzi ni nini? Hata watu wa karibu wa Kibaki wamemshauri hivyo, mmoja wapo ni Mwanasheria Mkuu wa Kenya bwana Amos Wako. Inaripotiwa pia kwamba nchi wahisani wametoa dukuduku lao.







Lakini kwa mujibu wa Gazeti la Standard la Kenya, Mwai Kibaki amekataa kuwa na serikali ya Mpito na kwamba wale ambao hawajaridhishwa na matokeo ya uchaguzi huo basi wafuate sheria, anasema hivyo huku akijua kuwa pengine ni sheria hiyo hiyo ambayo yeye ameikanyaga na kutoifuata kuingia Ikulu ya Kenya. Kwa jeuri na kiburi Kibaki anasema hivi "Wale hawataki kufuata sheria tutaonana na wao" Jamani tujiulize, kama aliweza kukusanya wanasheria kumwapisha 'fasta fasta' atashindwaje kuwakusanya kudhibiti hao anaowatuma kwenye vyombo vya sheria.







Huwezi amini, yaani ninapotafakari hayo nakosa cha kusema, si kwa sababu sina, bali moyo wangu unaumia, na ndipo ninapoanza kuwafkiria viongozi wengi wa Afrika, jinsi walivyo waroho! Wasio jali watu wao na wanafiki! Wengi na sio wote!




Sunday, December 2, 2007

Tanzania ilipata uhuru lini na kutoka kwa nani?

“Mnamo tarehe 30/06/07 kamati kuu ya utendaji ya Tanzania Association ilikuwa na kikao katika ofisi zake za muda zilizopo huko Tottenham London.Kati ya mengi yaliyojadiliwa ilikuwa ni kuadhimishwa kwa siku ya uhuru wa Tanzania na watanzania waishio hapa UK”

Hiki ni kipande cha taarifa ya Jumuiya ya Watanzania waishio nchini Uingereza kwenye mtandao. Angali kwa makini lile neno nililolikoleza kwa wino mweusi. Nilishtuka, nikajua kwa vyovyote kuna watanzania wengi wanaweza kuwa wanafikiri hivyo, kwamba Tanzania inasheherekea uhuru wake. Na hapa napenda ifahamike tu natoa maoni yangu ikiwa ni moja kati ya kusheherekea siku hiyo ya uhuru!

Siko hapa kuwabeza wala kuwadharau wale wenye mawazo kwamba Tanzania inasheherekea siku ya kupata uhuru! Kukaa kimya kunaweza kuchangia kuendelea kupotoshwa kwa historia, kwa hivyo kwa kutumia hekima, uungwana na busara ni vizuri tukakumbushana yale yaliyo ya muhimu kwa ajili ya historia ya nchi yetu.

Swali linaanza hivi, Je, ni kweli tunasheherekea uhuru wa Tanzania? Kuna ukweli hapo kihistoria? Ili kulijibu swali hili hebu tuanagalie maana ya Tanzania.

Tanzania ni muunganiko wa majina mawili ya zilizokuwa nchi mbili, yaani Tanganyika na Zanzibar. Nchi hizi mbili ziliungana mwaka 1964 na kuunda Jamhuri ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar, ambapo baadae ikaitwa Tanzania. Ikumbukwe pia kwamba, kabla nchi hizo hazijawa nchi moja Tayari Tanganyika iliyokuwa koloni la Mwingereza ilikuwa tayari imepata uhuru wake mwaka 1961, miaka miatatu kabla ya muungano huo.
Kwa hiyo wakati Tanganyika inapata Uhuru, nchi au kitu kinachitwa Tanzania hakikuwepo/haikuwepo. Zanzibar yenyewe ilikuja kupata uhuru wake kutoka kwa Sultani mwaka 1964 kwa njia ya mapinduzi. Kwa hiyo siku za uhuru wa Tanganyika kama nchi, na Zanzibar kama nchi pia ni tofauti. Kwa kusheherekea, Tanganyika ina siku yake ya uhuru na Zanzibar vivyo hivyo.
Kwa huoni kuwa kuna walakini kusheherekea uhuru wa Tanzania ambayo haijawahi kutawaliwa? Unapozungmzia Tanzania unazungumzia Tanganyika na Zanzibar, kwa nini tusheherekee uhuru wa nchi mbili tofauti, zilizopata uhuru kwa miaka na tarehe tofauti kabisa.
Sisemi haya kwa nia mbaya, ni kwa ajili ya wale wanaodhani tunasheherekea uhuru wa Tanzania. Hebu soma hii nayo hapa;
“Kuelekea maadhimisho ya miaka 47 ya Uhuru wa Tanzania Bara na 46 ya Jamhuri nimepata wazo. Angalia yale maneno yaliyokolezwa. Ni wakati wa kuiinua bendera yetu juu kama ishara ya umoja wetu na kama ishara ya utaifa wetu”
Huyu ni mchambuzi mahiri wa masuala ya kijamii hapa nchini, yeye anaishi nchini Marekani kwa sasa, anaitwa M. M. Mwanakijiji. Yeye kasema wazi kuwa ni uhuru wa Tanzania Bara, ni bora. Lakini hata hivyo kuna nchi inaitwa Tanzania Bara? Hili tuliache, tutalijadili wakati mwingine tukijaaliwa.
Kuna wakati niliwahi kusoma uachambuzi wa mwandishi fulani akihoji kwa nini historia ya Zanzibari inapotoshwa kuhusu mapinduzi, nadhani pia naanza kuona kuwa kuna mambo tukikaa kimya bila kuruhusu mijadala yenye kujenga tutaipoteza historia halisi na maana ya uhuru tulioupata.
Mwaka jana niliwahi kuhoji kwa habari hii ya Tanzania kuwa na sherehe za uhuru, lakini sikuzama kwa undani hivi, lengolisema hivi “Hivi ni uhuru wa Tanganyika au Tanzania ? Kwani Tanzania iliwahi kutawaliwa na nchi gain. Eti kwa mujibu wa walimu wang wa historian a kumbukumbu zangu, Tanganyika (si Tanzania ) ndio iliyopata uhuru mwaka 1961. Ni haki yangu kuhoji swali hili, ni muhimu, historia isipotoshwe. Naomba mhariri aruhusu mjadala katika hili. Kwa nini tusheherekee uhuru wa Tanzania badala ya Tanganyika ?” kama nilivyokwisha kusema kabla ni kuibua mjadala ili tuone kama tuko mahali sahihi au tumejisahau.
Bado swali langu liko pale pale, Tanzania kwa maana ya nchi, ilipata lini uhuru? Ilitawaliwa na nani? Kwa nini navyofahamu mwaka 1961, Tanzania ilikuwa haijazaliwa bado, kwa wale wanaotumia neno Uhuru wa Tanzania waache kufanya hivyo, kwani ni kupotosha historia, Tanzania haijawahi kuwa Koloni, Yaani tangu Tanganyika na Zanzibar ziungane na kuwa nchi moja, nchi hiyo (Tanzania) baada ya mwaka 1964 haijawahi kuwa chini ya Ukoloni.

Pengine kama tuna maana ya ukoloni wa kimawazo (kifkra) na kiuchumi, kwamba bado tunatawaliwa kiuchumi na kifikra na mataifa ya Magharibi. Ndio maana tunaendekeza hadi lugha yao na kuona kiswahili ni takataka na laana kwetu. Ndio maana asilimia 40% ya bajeti yetu tunategemea kutoka kwao. Hata kama ndivyo, kwamba tunatawaliwa kiuchumi na kifikra je uhuru tumeupata? Lini, tarehe ngapi?

Lakini pia hivi hamfikirii kwamba kuendelea kusheherekea uhuru wa Tanganyika ni kuendelea kuitambua Tanganyika? Wana makosa gani sasa wakina Mtikila wanapojinadi kuwa wao si watanzania, bali watanganyika? Kwa nini tusisheherekee tu uhuru wa Tanzania kama upo au tubakie tu na sherehe za Muungano ambao nao una mkanganyiko?

Chonde ndugu zanguni, popote mlipo,lengo langu ni kuwakumbusha wale wanaopenda kutumia neno uhuru wa Tanzania badala ya Tanganyika, na tena nimesema kwamba kama tunasheherekea uhuru wa Tanganyika ina maana kwamba tunakiri na kuungana na kina Mtikila kwamba bado kuna nchi inaitwa Tanganyika, je Katiba inasemaje? Je tuna katiba ya Tanganyika bado? Siku moja nitaleta uchambuzi kuhusu suala la Muungano, ili ujue kwamba kuna mambo mengi bado tunayafanya lakini huku tukiwa hatuelewi bado maana yake au yakiendelea kutuchanganya! Lazima tufanye haraka kurekebisha ili vizazi vijavyo visije vikatuhukumu.

Wednesday, November 21, 2007

Ni kweli wanatafuta vipaji au wanawadhalilisha vijan wetu?

Unaona hawa? Hawajali jua wala mvua, tena wengine hawajaaga hata makwao, wanawania gari na kurekodi bure! Angalia wale wengine wamechoooka, nani akumbuke kuwapa viti vya kupumzikia wakati shida ni yao wenyewe? Kwani walifungwa kamba kuwa ni lazima waje?
Hebu angalia hawa nao, kwa haraka haraka wako zaidi ya hamsini hapa, lakini pia wanajua kuwa anatakiwa mmoja tu kushinda, kwa kweli wengi wao wanasubiri kwenda kuambiwa hawajui kuimba bila kuambiwa ni kwa nini au ni mapungufu gani waliyonayo! mmh! Watatoka wamenuna badala ya kufikiria namna nyingine ya kutoka bila mgongo wa BenchMark! haya bwanaa!!

Huyu ni Salama jabir, ni mtangazaji wa TV na redio kule Dar es salaam! Naye ni mmoja wa majaji wa kuchagua mwanamuziki bora wa Tanzania!


Huyu ni John Kitime, meneja wa Kilimanjaro Band.

Huyu ni Joachim Kimaryo, wengi humuita Master J, yeye naye ni mmoja wa Majaji




Huyu anaitwa Rita Paulsen ni mkurugenzi wa BenchMark LTD, waandaaji wa shindano, eti naye ni jaji. Mumy usijisikie vibaya, mimi ni mwanao, natoa tu maoni yangu, nakupenda sana!







Si vibaya nikitoa utabiri wangu kinachoweza kutokea mwishoni mwa makala hii. Kwamba wako wale watakaoniona mmoja kati ya waleeee waliopitwa na wakati, siwazuii kufanya hivyo, huu ndio ulimwengu wa Utandawazi, tuliyataka wenyewe, kila mmoja anatoa lake, ndio maana huoni nguvu ikitumika sana kuzuia mmomonyoko wa maadili, yote ni utandawazi! Upoo?

Nataka kuua ndege wawili kwa wakati mmoja, naandika kuhusu kile kinachitwa ‘Big Brother Africa’ na ‘Bongo Star Search’, nianze na lipi hapa? Naanza moja kwa moja na Bongo ‘Star search’

Haya ni mashindano au Kampeni? Vyovyote lakini mwisho wa yote wahusika wanasema kuwa wanataka kumpata mwimbaji mahiri/nyota wa Bongo yaani Tanzania. Wanaalikwa watanzania weeengi, na hasa vijana, lakini mwisho wa siku anatoka mmoja. Sijui kwa wengine, lakini kwa upande wangu sikua navutiwa na kampeni hii, nilikua nikisikia tu kuwa kuna kipindi kama hicho kinachorushwa na kituo cha ITV.

Lakini jumapili iliyopita nilitaka nikae nione kinachofanyika, jinsi nyota huyo anavyosakwa, ndipo nilipojionea kile kipindi, na mwishoni kichwa changu kilijaa maswali na tafsiri nyingi sana.

Niliangalia wale vijana wanaojipitisha mbele ya wale wanaoitwa majaji (Salama Jabir, John Kitime, Rita Paulsen na Joakim Kimaryo au Master J) Kwa haraka haraka tu niseme mapema kwamba sikuwaelewa wale majaji, sikuelewa vigezo vilivyotumika kuwapa nafasi hiyo ya ujaji.
Ngoja nikuambie kwa nini nasema hivi;
Rita Paulsen yeye ni Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni iliyoandaa shindano hilo, Benchmark Productions Ltd, hatujawahi na wala haijulikani ni wapi na lini alikuwa muimbaji/mwanamuziki kiasi cha kuwa na sifa za kuchagua wanamuziki tena nyota wa Tanzania. Kuwa bosi wa kampuni inayoandaa muziki si kuwa mwanamuziki!

Salama Jabir
Salama Jabir, yeye ni mtangazaji wa kituo cha East Africa Radio na Channel 5, ambao ni ndugu na Bench Mark, anafahamika na wengi kuwa si mwanamuziki hata ukisiliza tu sauti yake. Tuendelee! Inashangaza kama kigezo cha utangazaji kinampa sifa ya kutafuta na kumpitisha mwanauziki nyota wa Tanzania.


Master J yeye ni mtayarishaji wa muziki, si mtunzi wala muimbaji kwa anavyofahamika na wengi.
John Kitime, huyu ni mwanamuziki na meneja wa bendi ya Kilimanjaro, lakini ni jaji anayeonekana kutokua na sauti katiaka maamuzi ya shindano hili tofauti na wale wasio wanamuziki, yaani Slama, Rita na Master J.

Kwa hiyo tukiamua kuwa makini, katika shindano hilo kuna jaji mmoja tu ambaye ni kitine kwa maana ya taaluma yake.

Jambo lingine lililonisumbua ni kwamba, hata kama wangekuwa ni majaji, je, wanatumia vigezo gani kumpata mwanamuziki wanayemtafuta? Je ni unyororo wa sauti? Ujumbe katika nyimbo? Madoido ya kucheza? Au nyimbo tu wanazozipenda majaji ambazo zimewahi kuimbwa na wanamuziki wengine?

Katika suala la majaji, waandaaji wangeiga mfano wa Mamu pale kariakoo ambapo yye huwatumia wanamuziki waliokubalika zaidi kili kuzipitia na kuzijaribu kazi za wanamuziki wanaoinukia!

Hata hivyo, suala lingine ni kwamba waandaaji wa shindano hilo nao wanaumwa ule ugonjwa wa kuendekeza utamaduni wa nje hasa suala la lugha, wanajua fika kuwa wanamtafuta mwanauziki nguli wa Tanzania, na sio Marekani wala Hispania, lakini ajabu ni kwamba mpaka jina la shindano ni la kizungu, ndilo linalotumika kutangaza kwenye vyombo vya habari, kuna ubaya gani kuliita shindano hilo, SHINDANO LA KUMSAKA au KUMTAFUTA MWANAMUZIKI NYOTA WA TANZANIA? Hata kama ni refu, lakini si ndio lugha yenu? ukiangalia majaji wamekuwa mahodari kwenye kushangilia nyimbo za magharibi, za kizungu, kwa hiyo kama vizazi baadae vitakuja kusaka na kuhumu wahumu wa utamaduni wa Tanzania hususani kwenye lugha, BENCHMARK LTD hawawezi kukwepa hukumu hiyo!

Kwa taarifa tu ni kwamba huo ulikuwa ni utangulizi wa makala hii kuhusu Bongo Star Search! Shindano lisilo na vigezo!

Lakini binafsi nimejifunza kwa watanzania wenzangu hasa vijana, na nimegundua na kuendelea kujua kwamba dezo au vya bure vitaendelea kutumaliza tusipo kubali kugeuka. Maradhi ya kupenda dezo ni mardhi yaliyolikumba hata Taifa letu, kuendelea kutegemea hisaniza Wazungu katika kujenga uchumi wetu, wakati tuna mbuga, mito, bahari, milima na wataalamu mbalimbali.

Nina maana gain? Wengi walioenda kujipitsha mbele ya majaji ili kuchaguliwa wana uwezo mkubwa wa kufanya mazoezi yao ma kuja kuibuka kuwa waimbaji mahiri bila hata ya kupitia BenchMark, na hivyo kuepuka na kukwepa udhalilishaji wanaofanyiwa na majaji na ule wanaojifanyia wenyewe. Aliyekaa kwa makini na kufuatilia kipindi kile atagundua kuwa uamsikini au unyonge na dezo ndio iliyowapeleka wengi pale leaders club ili kubahatika kuchaguliwa! Masikini vijana watanzania, wanaenda pale na kukutana na watu kama Salama jabir ambaye haangalii kama wewe una wadogo zake kama yeye, au umemzidi kwa namna moja ama nyingine na kukujibu hovyo! Nimeona vijana wengi wakidhalilishwa bila wao kushituka, lakini siwalaumu ni kuna nadharia kadhaa hapa, kwanza umasikini au dezo na kutaka umaarufu wa haraka!

Wanachokimbilia wengi ni kupata mkataba wa kurekodi albamu zao bure, pesa (kama zipo) na gari la bure! Sielewi kwa nini wasikubali kuwa masikini jeuri, kwamba kama mtu ameamua kukusaidie hebu na afanye hivyo bila kukusimanga na kukudhalilisha, vinginevyo tafuta kutoka kivyako!

Ninayo mifano ya wanamuziki kama Ephraim Mwansasu, faustine Munishi, Neema Mushi, Bahati Bukuku, David Nyanda, Sipho Makabane, Jabu na wengineo wa ndani na nje ya nchi ambao walisota sana kaba ya kutoka! Matokeo ya kutegemea mashindano kama haya ambako utaambiwa hujui kuimba wakati unajua ni kujichelewesha mwenyewe na kwenda kuvunjika moyo na kuacha kuchochea kipawa chako! Si ajabu kwamba hata wale amabo wamepitishwa na watu wengine si waimbaji ka wewe uliyekatishwa tama kwa kuambiwa na Master J au Salama, au Rita kuwa hujui kuimba!

Nakumbuka wakati nilipokuwa nataka kufikisha makala zangu magazetini waliponiambia kuwa sijui kuandika, niliamua kuandika kwenye madaftari ya shuleni na kuyahifadhi, kasha nikiwa kidato cha sita nikaomba walimu waniruhusu nianzishe kagazeti kangu, humo nikawa naandika mawazo yangu na kufikisha kwa wanafunzi wenzangu, mara nyingine niliwahi kufika shule mapema na kuweka ujumbe wangu kwenye ubao wa darasani, ni mpaka mwalimu alipofika ubao ulifutwa! Sasa ninaweka maandishi yangu kwenye blogu, tembelea www.amkenitwende.blogspot.com , sisahau pia kwamba niliambiwa na wazazi wangu kuwa sina sauti nzuri ya kuimba, sikukubali, nikaacha kuimba mbele za watu, nikawa naingiza sauti kwenye kaseti, mpaka watu Fulani waliponiona na kutaka nikarekodi nao, hata hivyo mambo hayajakwenda sawa, masomo yamenibana, lakini nitarekodi, sasa naandika nyimbo na nawapa wengine wanazitumia! Sikukubali!

Kama moto wa kuimba unawaka ndani endelea kuimba, wakati unaoga au wakati unavaa suruali au sketi yako chumbani, imba usiogope, imba sio mpaka Salama Jabir au Master J akuone, sio mpaka BenchMark wakuone!

Usikubali watu watumie kukosa kwako pesa ya kurekodi wakudhalilishe, na usikubali kudhalilika, kuna njia nyingi za kutoka kimuziki, muweke Mungu mbele, enzi za kina Munishi, Mzungu Four, Patrick Balisidya, Msanii Kyande, Charles Jangalason hakukuwa na BenchMark LTD na bado walitoka!
Itaendelea wiki ijayo!

Sunday, November 18, 2007

Fumbo, kitendawili na hadithi pamoja?


Mheshimiwa Zitto Kabwe

Kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza rais Jakaya Kikwete kwa uamuzi wake wa kuunda tume ya kuchunguza suala zima la mikataba ya madini nchini, na napenda ifahamike kuwa pongezi hizi ni za dhati kwa maana ya kutoka moyoni, tena kule kilindini. Pongezi hizi ni kwa sababu mbili.

Kwanza ni kwa sababu ya rais kutimiza ahadi aliyoahidi hivi karibuni katika mkutano mkuu wa CCM pale Dodoma , aliahidi kufanya hivyo, naam amefanya tena kwa muda mfupi sana , ametimiza ahadi.

Lakini la pili lililokubwa zaidi ni kwa vile rais anaelekea kupona ule ugunjwa wa siku nyingi wa serikali ya CCM kufanya mambo kwa kuzingatia maslahi ya chama zaidi kuliko Taifa, uginjwa wa kudhani wapinzani hawawezi kutoa mchango wowote kwa serikali iliyoko madarakani zaidi ya kupiga kelele za majukwaani na kupoteza muda, hiyo ndio ilikuwa pengine ni dhana ya CCM na serikali kwa ujumla.

Lakini Kikwete ananishawishi nianze kuamini kuwa CCM ( kama si dhamira binafsi ya Kikwete) inaelekea kupona uginjwa huu, ni pale alipoamua kuunda tume inayojumuisha viongozi wa CCM na wale wa upinzani wakiwamo John Momose Cheyo wa UDP na Zito Zuberi Kabwe wa CHADEMA. Kwa moyo mkunjufu nasema hongera sana Mheshimiwa rais na asante !

Hata hivyo mwishoni mwa makala hii nitakutaka mpendwa msomaji wangu uamue/upembue uteuzi huu, ikiwa ni fumbo, kitendawili au hadithi kwa maana ya historia mpya ambayo vizazi vitasimuliwa hapo baadae?

Tume hii imekuwa gumzo mitaani na hasa kwa wafuatiliaji wa masuala mbalimbali hapa nchini, na aliyesababisha gumzo hilo si mwingine ni Zitto Kabwe, suala sio tume, suala ni Kabwe kuwa kwenye tume hiyo. Wakati gumzo hilo likiwa bado bichi, gazeti moja likaripoti kuwa baadhi ya wanachama wa CHADEMA wamanza kumjadili Kabwe, kwamba inakuwaje awe kwenye tume hiyo na mambo mengine mengi ambayo nimeyatafsiri kama ya kitoto kama sio propaganda za baadhi ya maadui wa Zitto Kabwe kupitia magazeti hayo. Suala la Zitto kabwe kuwa kwenye tume hiyo siyo suala la kiitikadi, ni swala la kitaifa.

Mimi sijui kwa upande wako unafikiriaje, wenzako wanasema Zitto Kabwe ana ajenda ya siri na CCM, kwamba ananunuliwa ili kuzibwa midomo, mimi nayakataa madai haya kwa nguvu zote, ni utoto wa kimawazo kuanza kufikiri hivi mapema, tusiache kujadili hoja ya msingi, tukianza kujadili uhalali wa Kabwe kuchaguliwa na rais anayetokea CCM tutawapa walfi nafasi ya kupumua kama wapo.

Na hapa leo nataka nikutafakarishe wewe mwenye mawazo hayo ya kitoto kuhusiana na uwepo wa Kabwe kwenye tume ya rais.

Unakumbuka kuwa Zitto Kabwe alifungiwa na Bunge (spika?) kuhudhuria vikao vya bunge kwa madai ya kulidanganya bunge, kwamba alitoa madai ya uongo, wengine wakafika mbali kwamba amemdhalilisha Waziri Karamagi? Unafikiri hii ina maana gain? Sikiliza wewe! tungeweza kumwita Kabwe ni mhalifu aliyeko kifungoni, lakini mpaka anatoka bungeni alisisitiza kuwa madai yake yalikuwa kweli, na akasema anawaachia wananchi wengine waamue, kwamba yeye alikuwa amemaliza zamu yake. Bunge likazodolewa na kushutumiwa na wanasiasa, wanaharakati na wananchi wengine wa kawaida. Ninakumbuka wakati ule nilikuwa Mbeya, nilipigiwa simu na mwanafunzi mmoja wa sekondari iliyoko Morogoro, huyu msichana alisema hivi, “niliiheshimu sana CCM, lakini sasa kwa hatua ya Bunge kumfungia Zito Kabwe, mh, mimi nahamia CHADEMA” Nilichomshauri ni kutulia ili afanye maamuzi sahihi, kuhama chama kusingemnusuru Zitto Kabwe wakati ule.

Zitto Kabwe aliitwa muongo, mzushi, wakasema anajitafutia umaarufu kwa kusema uongo, mjidala hiyo ikafika hata vyuoni na kuwagawa wanafunzi, wengine wakimtetea huku wengine wakimshutumu na kumwita kimbelembele, Zitto akasonga mbele, vyama vya upinzani vikachochea moto kwa kuamua kupanga ziara za kwenda kuishitaki serikali kwa umma, maana bunge lilishindwa kuidhiti serikali.

Mbele ya macho ya bunge Kabwe alikuwa ni mhalifu aliyeko kifungoni, kadhalika mbele ya Karamagi na Kikwete na baadhi ya wana CCM, sina shaka kwamba adhabu ya bunge kwa Zitto ilimfariji sana Karamagi aliyemwita Zitto Kabwe kuwa ni muongo na mdhalilishaji.

Wiki iliyopita limetokea jambo, sijui mpaka saa niliiteje, ninakupa nafasi ya kutoa jina. ‘Mhalifu’ yule yule, muongo, mzushi na mdhalilishaji aliyefungiwa kwa misimamo yake kwenye kulinda rasilimali za Taifa na hasa madini, leo amekuwa wa maana mbele ya rais hata kupewa ujumbe katika tume yenye kazi ya kuchunguza suala lile lile la madini. Unasemaje? Je, rais kapitiwa au anajua kwa hakika alichokifanya? Hajui kuwa Zito ni mfungwa? tena kwa sababu ya kutetea madini ya nchi yetu, madini ambayo yamefanya serikali ipoeze imani kwa wananchi wake? Rais amesahau kuwa waziri wake (Karamagi) anamchukulia kuwa Zito Kabwe ni muongo na mzushi? Kwa nini kaamua kumteua? Je, Zitto Kabwe ni msafi tofauti na anavyoonekana mbele za macho ya bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania ?

Je Zito Kabwe ni mkweli tofauti na fikra za Karamagi? Au kwa nini rais amemteua? Kwetu tunaamini kuwa mheshimiwa rais kazingatia na kuamini kuwa Zito Kabwe anafaa na anaiweza kazi aliyompa, kigezo cha uadilifu, uchapa kazi, ukweli na uwazi ndicho kilichompa kibali zito mbele za rais Kikwete.

Kama ndivyo basi, tuiteje uteuzi huo, ni fumbo la rais kwa Karamagi na bunge? Kwa maana kwamba bunge na Karamagi walivyomfikiria Zitto Kabwe sivyo alivyo? Au ni vipi? Kama ndivyo, je rais amemsuta Karamagi? Kwa hiyo kama ni hivyo, huo si ushindi wa kishindo kwa Zitto Kabwe kama mwanaharakati, kwamba sasa imethibitika kuwa alikuwa ni Nabii asiyeheshimika na kutiliwa mashaka bure tu!

Je hatuwezi kufikiri kuwa CCM na serikali yake imejizodoa? Mimi huko simo, ni katika kujaribu kuwaza na kuwazua, lakini pongezi zangu kwa rais zinabaki palepale!
Ni vipi pia? Uteuzi huo ni kitendawili? Nani atakitegua? Kinasemaje hicho kitendawili? Je ni hadithi mpya katika historia ya Tanzania ?

Suala la Zito kwenye tume hiyo limenikumbusha habari za RADA, wanaharakati walipotuhumu kuwa ina mazingira ya rushwa, baadhi ya wanunuzi wakapinga kwamba sivyo ilivyokuwa. Leo TAKUKURU imemtangaza mmoja wa watuhumiwa hao wa rushwa hadharani, hii ina maana kuwa mazingira ya rushwa yalikuwapo, je wanasemaje wanaposikia kuwa madai ya wale walioitwa wazushi yamethibitika kuwa na ukweli?

Naamini hili ni funzo hata kama rais amefanya bila kujua kuwa kuna watu wangekuja na tafsiri nyingi sana baada ya uteuzi huo.Kwa hiyo tunashawishika kuamini kwamba, kumbe kuna madai mengi ya wapinzani yakiwemo yale ya ufisadi tutakuja kuujua ukweli wake siku moja, tena watakaokuja kuuthibitisha ni hao hao wahusika, tuombe Mungu!

Kila la Heri tume ya rais!

Monday, October 29, 2007

KWA HERI SHUJAA LUCKY DUBE!


NITAMKUMBUKA LUCKY DUBE SIKU ZOTE ZA MAISHA YANGU!





KWA HERI SHUJAA LUCKY PHILIP DUBE



Natafuta namna ya kuanza kuandika makala hii, kwa sababu nataka iwe makala maalumu kabisa, na zaidi sana nataka iwe tuzo kwa kazi ya nzuri ya Lucky Philip Dube wakati wa uhai wake duniani. Mbali na serikali ya Afrika ya kusini kumzawadia kombe la dunia la Rugby ambalo nchi hiyo ilitwaa baada ya kuifunga Uingereza, nataka makala hii iwe pia zawadi ya rambirambi kwa familia ya mwanamuziki huyo na Afrika kwa ujumla.

Unaweza ukauliza pengine, kwamba kama makala hii inamhusu Lucky Dube kwa nini basi isiwe kwenye kurasa za michezo na burudani? Sikiliza ndugu yangu, kwa upande wangu mwenzako Lucky Dube hakuwa mwanamuziki na mleta burudani, kwangu dube alikuwa ni mwanaharakati kama wanaharakati wengine duniani. Ndio maana inawashangaza watu kuona Mwinjilisti kama mimi kuanza kuzungmzia habari za Lucky Dube, na uzuri sikumficha mtu, nilisema wazi nimefiwa, nimeumizwa na kifo cha ndugu huyu wa Afrika.

Nilishaacha kusikiliza nyimbo za Lucky dube, na badala yake mpaka mauti ina mkuta nilikuwa nikizisoma na kuzitafakari, zilikuwa kama hotuba za kiongozi Fulani kwangu, nilimchukulia sawa na kina Nelson Mandela na kina Martin Luthere King, Jr.

Kuna mambo mengi yanayonifanya nimtofautishe Dube na wanamuziki wengine na hasa wale wa rege, kwa mfano matumizi ya bangi, pombe na imani kwamba haile Selassie alikuwa au ni Mungu, haya na mengine yalinifanya nimheshimu Dube na kumtenga na baadhi ya wanamuziki wenzake wakiwemo wa Tanzania. Nimewahi kubishana sana na wenzangu kuhusu imani ya Dube, hasa nilipokuwa shule ya msingi pale Gilman Rutihinda pale Dar es salaam, wengi waliamini kwamba, eti kwa sababu tu alikuwa na rasta kichwani, basi yeye ni ‘rastafarian’ na pia kwamba kwa sababu aliimba rege, pengine ni kutokujua kwamba rege ni aiana ya mahadhi Fulani ya muziki na kwamba hakuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya rege na bangi, mimi niliamini kuwa Dube ni mkristo kwa dini, nah ii ilitokana na baadhi ya maneno ya baadhi ya nyimbo zake, kigezo kingine ni kwamba nyimbo nyingi za Lucky Dube zimeakisi ukweli kuhusu maisha yake mwenyewe aliyoyapitia.

Fuatilia nyimbo kama slave, remember me, think about the children na it’s not easy, katika mabishano hayo jamaa zangu waliendelea kushikilia misimamo yao ile, lakini Lucky Dube mwenyewe alipokuja Dar mwaka 1997 aliwahi kusema hivi “kama urastafarian ni kufuga rasta, kuvuta bangi na kunywa pombe na kuamini Haile Selassie ni Mungu basi mimi si Rastafarian, lakini kama ni itakuwa ni kuhusu siasa na maisha ya kila siku basi mimi ni Rastafarian”

Kwangu tofauti kubwa iliyoko kati ya Lucky Dube na wanaharakati na wanafalsafa wengine kama Mwalimu Nyerere wa Tanzania, Nelson Mandela, Martin Luther na wengine ni kwamba wao walikuwa hawaimbi lakini wote walitumia majukwaa kueneza ujumbe kwa hadhira yao na malengo yao yalifanana, wote ni wapambanaji, kama huamini sikiliza kauli aliyoitoa Dube mwaka 2000, hapa anasem,a hivi “A lots of people were thinking that once we had this black government everything would be fine, may be we were only fighting the past government because it was a white government. But that is not the case with me, I was just fighting the system, it is the same now, if there is injustice or any sort of nonsense towards people I will sing about that” akiwa na maana kwamba, watu wengi walifikiri kwamba baada ya kuwa na serikali ya watu weusi kila kitu kinge kuwa sawa, pengine tulikuwa tukipambana na tu na serikali ya zamani kwa sababu tu ilikuwa ni serikali ya weupe (Makaburu) lakini sivyo ilivyo kwangu, nilikuwa napambana na mfumo, na ndivyo ilivyo sasa, kama kuna namna yoyote ya uonevu na upuuzi wowote wanaofanyiwa watu (raia) nitaimba hilo nalo”

Hii si kauli ya mtu wa kawaida, ni kauli inayoweza kutolewa na wanaharakati jasiri tu kama Lucky Dube, na ukiwa makini utagundua kupitia kauli yake kwamba hakuwa mpigania haki wa Afrika tu bali pia wa Ulimwengu. Anasema ili mradi serikali hiyo inafanya ndivyo sivyo dhidi ya wananchi wake yeye ataimba. Na kupitia Dube ndipo pia unaweza kuona umuhimu wa kuwa na wagombea binafsi wa kizalendo, wao mara nyingi hawana muda wa kusiamam na kutetea maslahi ya vyama vyao au serikali za dhalimu, maana hata kama wangetaka kusiama upande wa wananchi katiba au kanuni za vyama vyao zingewabana. Hujawahi kusikia wanasiasa wanaolalamikia au kukosoa mwenendo mbaya wa vyama dhidi raia wao wanaambiwa apaleke hoja zake kwenye vikao? Wanafanya hivyo huku wakielewa fika kwamba wataminywa na kunyamazishwa. Sijaelewa hasa kwa upande wa Tanzania kwa nini bado kuna ugumu kuruhusu wagombea binafsi kama walivyo dai watu kama Faustine Munishi na Christopher Mtikila, wanahofu kitu gain?

Lucky Dube aliimba na kusema ukweli bila kuogopa Taifa, chama au serikali Fulani. Fuatilia wimbo kama Puppet masters, No truth in the World, Victims, na You stand alone utalewa nini nasema hapa.
Fuatilia wimbo wake wa 'Crazy World hapa uone
So far so good we still living today
But we don't know what tomorrow brings
In this crazy world
People dying like flies every day
You read about it in the news
But you don't believe it
You'll only know about it
When the man in the long black coat
Knocks on your door'Cause you're his next victim
As you are living in this
Chorus:Living in, living in this crazy world (x4)
Leaders starting wars every time they want
Some for their rights,
Some for fun and their own glory
letting people die for the wrong that they do
Oh it's painful
come on now little boy
Say your prayers before you sleep
Little boy went down on his knees
And he said:"Oh Lord Now I lay me down to sleep
I pray the Lord my soul to keep
And if I die before I wake
I pray the Lord my soul to take.
"'Cause he's living in this crazy worldOh Lord
Mpaka hapa sasa angalau tunaishi, lakini hatujui kesho italeta nini,
Katika ulimwengu huu uliochanganyikiwa,
Kila siku Watu wanakufa kama inzi,
Unayasoama haya kwenye taarifa za habari lakini huamini,
Unakuja kujua mpaka pale mtu mwenye koti jeusi anapokujia
Na kugonga mlangoni kwako, Kwa sababu wewe ndiwe mhanga wake
Unapoishi kwenye ulimwengu huu ulio changanyikiwa
Viongozi huanzisha vita kila wakati wanapojisikia,
wengine wa kutetea haki zao na wengine kwa ajili ya mambo ya ajabu na kujitafutia tu utkufu
Wanaaacha watu wanakufa kwa amakosa wanayofanya wao, Ooh inaumiza
Ee mvulana mdogo, fanya sala kabla hujalala, Yule kijana akapiga magoti na kusema,
Ee Bwana Sasa nalala, Namuomba Bwana roho yangu ailinde, Na kama nitakufa kabla sijaamka
Namumba Bwana roho yangu aichukue, Kwa sababu anaishi kwenye ulimwengu huu uliochanganyikiwa!

Lucky Dube aliwashinda hata baadhi ya wanasiasa kwa moyo wa upendo kwa watu wake, na kwa moyo huo ndio maana mmoja wa mawaziri nchi Rwanda katika salamu zake za rambirambi amesema wamempoteza rafiki yao . Ni nadra sana kwa viongozi wa kitaifa kutoa kauli zao kwenye vifo vya wana muziki wengie wa kawaida, ndio maana nakwambia kwa watu wanaofuatialia masuala ya kiutawala, haki na usawa watakubaliana na mimi kuwa Dube hakuwa tu mwanamuziki bali mwanaharakati hasa, hilo linaweza lisisemwe wazi au hadharani na wanasiasa lakini wanaelewa mishale yake, nah ii ni hasa kwa wanasiasa wakorofu, waonevu na wadhalimu dhidi ya wananchi wan chi zao. Dube alikuwa makini kwa maana ya kuijua historia ya Afrika na jamii yake.

Alitembelea Rwanda mara tu baada ya mauaji ya halaiki mwaka 1994, mauaji ambayo hayatasahaulika kwa vizazi hivi vya karibuni, huko alifanya maonesho kwenye jiji la Kigali kwenye uwanja wa mpira wa Amahoro (Amani) na moja kati ya nyimbo zilizowatoa Wanyarwanda machozi ni ule wa ‘together as one’ sehemu ya wimbo huo inasema hivi


In my whole life,My whole life I've got a dream (x2)

Too many peopleHate apartheid Why do you like it? (x2)

Chorus: (x3)Hey you rasta manHey European,Indian man, We've got to come together as one

Not forgetting the Japanese


The cats and the dogsHave forgiven each otherWhat is wrong with us (x2)All those yearsFighting each otherBut no solution (x2)


Kwa kiswahili anasema. Katika Maisha yangu yote nimekuwa na ndoto, watu wengi hawapendi ubaguzi wa rangi, kwa nini wewe unapenda, enyi marastafariani, wazungu na wahindi tunatakiwa kuwa kitu kimoja

Paka na mbwa walisameheana, tatizo ni nini kwetu? Miaka yote hii tumepigana wenyewe kwa wenyewe bila suluhisho,


unaonaje wewe ujumbe huu, je haukuwa mahususi kwa Wanyarwanda kwa wakati ule? Bila shaka aliimba pia ule wimbo wake wa “we cray for peace’ (tunalilia Amani)
Katika wimbo huo anasema “tunalilia Amani kamili, Ee Mungu tunalilia upendo katika ujrani huu, nakwambia hakuna maji yanayoweza kuzima moto huu (vita) Ni Mungu peke yake anaweza kutuokoa”
Kuanzia wiki ijayo nitakuletea maelezo na tafsiri ya baadhi ya nyimbo zake kwa wiki mbili ikiwa ni ishara ya watoto wawili wa Dube walioshuhudia mauja ya baba yao.

Dube pia atakumbukwa na watu masikini duniani kwa sababu ya kuwatetea, aliwashukia matajiri wa ulimwengu kwa kusema utajiri wao hakuwa na maana yoyote duniani kama watakuwa hawawajali masikini na wale watu wasio na matumaini katika wimbo wake wa ‘hand that giveth’
Sasa LUCKY PHILIP DUBE hayupo tena, wamekatisha uhai wake kwa risasi, mtu ambaye pamoja na kwamba hakunifahamu nilimuombea ampe Yesu maisha yake, niliwahi panga siku moja kwamba siku za usoni ningemtembelea Afrika ya kusini ili kumshirikisha neno la Mungu, sasa katoweka na ndoto zangu zimezimika. Naanza kurudi nyuma kukumbuka jinsi alivyonifanya nitoroke shule kwenda kumpokea uwanja wa ndege Dar es salaam na alipokuwa anaorudi kwao nilitega shule kuhakikisha kuwa naenda kumuaga, nakumbuka nilipokuwa nagombana na mama nyumbani kwa sababu ya kupiga kanda zake mfululizo na kuziimba pia kwa sauti, nakumbuka nilipogombana na walimu kama vile mwalimu Sadala na mwalimu Assey pale Rutihinda kwa kutembe kila wakati huku nikiimba nyimbo za Dube, nilipotumia nyimbo zake kama mifano katika mazungumzo na rafiki zangu na katika baadhi ya makala zangu, Bila shaka wakina Simba Ramadhani, George Madanga, Hafidh Ismail, Juma, Humphrey Mutabirwa na Ukasha Mrami wanakumbuka nilivyokuwa kituka kwa kuwehuka na mwanaharakati huyo, ndio maana pamoja na kuelewa kwamba hivi sasa mimi ni mchungaji bado hawajaacha kunitumia salamu za pole! Hayupo tena! Tuonane wiki ijayo kuendelea na maombolezo na kumbukumbu hii muhimu katika maisha yangu!